Kusah Adokeza Ujio Wa Collabo Kati Yake Na Ruby

Image Source: Online 

Writer: Charles Maganga 

Msanii nguli kunako kiwanda cha Bongo Fleva, Kusah hivi karibuni amedokeza kuwa huenda kuna collabo inakuja baina ya msanii Ruby.

Kusah na Ruby ukiachana na kwamba ni wasanii lakini pia ni wazazi wenza ambao wana mtoto mmoja japo kwa sasa wametengana.

Akizungumza kwenye mazungumzo ya hivi karibuni, Kusah amedokeza kuwa kuna kipindi Ruby alimtafuta ili waachie collabo yao waliyofanya pamoja na Kusah aliongeza kuwa pamoja na tofauti zao za hapo awali lakini yeye binafsi alikubali ujio wa collabo hiyo

"Alinicheki Ruby aliniomba kuna nyimbo tulifanya zamani, kwamba anataka kuitoa. Ilikuwa ni sawa tu, tuliongea kibiashara na tulielewana" alizungumza Kusah

Ikumbukwe kuwa Kusah na Ruby tayari wameshatoa ngoma nyingine za pamoja ikiwemo "Kelele" pamoja na "Dondosha"

Leave your comment