"Next Level Imenirudisha Nyuma Kimuziki" - Bando MC

Image Source: Online 

Writer: Charles Maganga 

Msanii na rapa anayefanya vizuri kwenhe kiwanda cha muziki Tanzania, Bando MC hivi karibuni alifunguka jinsi ambavyo Next Level Music, lebo inayomilikwa na Rayvanny ilivyomrudisha nyuma kimuziki.

Bando ambaye alianza muziki mwaka 2019 alidai kuwa Next Level Music imechangia kwa kiasi kikubwa kumrudisha nyuma kimuziki kwani alifikia hatua ya kusaini mkataba na alisubiri zaidi ya mwaka na nusu lakini hakuna kilichofanyika.

Bando aliongeza kwa kusema "Mimi nimekaa pale Next level zaidi ya mwaka mmoja na nusu, Mimi nimetoka pale mwaka 2022 Broo alikuwa mtu wangu wa karibu kabla ya kuanzisha hiyo lebo nilikutana nae IG aliniambia inabidi tufanye kazi na alinikuta tayari nimeshafika sehemu" 

Leave your comment