Harmonize Atangaza Kupigana Ndondi Na Mwanasumbwi Hassan Mwakinyo

Image Source: Online 

Writer: Charles Maganga 

Kama ulidhani msanii nguli kutoka Tanzania, Harmonize yuko vizuri kwenye suala la kuimba pekee basi taarifa mpya ni kwamba msanii huyo hivi karibuni amedokeza kuwa pia yupo vizuri kwenye mchezo wa ngumi.

https://mdundo.com/song/2785338

Harmonize ametangaza kuwa hivi karibuni ataingia ulingoni kupambana na Hassan Mwakinyo ambaye ni moja wapo ya wanamasumbwi bora wa muda wote nchini Tanzania.

Harmonize alitoa hiyo kuptia Instagram mara baada ya kuchapisha mazungumzo yake na Mwakinyo wakiwa DM ambapo wawili hao walitambiana, kila mtu akimtishia mwenzake kuwa ni bora zaidi.

Mvutano huu wa maneno baina ya Harmonize na Hassan Mwakinyo unakuja siku chache tangu Harmonize atangaze kuingia kwenye mchezo wa ndondi.

 

Leave your comment