Gigy Money Afichua Kiasi Alicholipwa Na Harmonize Kwenye Video Ya "Dharau"

Image Source: Online 

Writer: Charles Maganga 

Kama umeshaitazama lyrics video mpya ya Dharau kutoka kwa Ibraah akiwa amemshirikisha Harmonize, basi bila shaka ulimuona msanii na socialite maarufu kutokea Tanzania, Gigy Money.

Hivi karibuni, Gigy amefichua kuwa Harmonize alimlipa kiasi cha Tshs Milioni 5 ili aweze kushiriki kwenye video hiyo. 

Gigy Money alifichua kuwa, kwa mara ya kwanza alipendekeza kulipwa Milioni 10 lakini mwisho wa siku walikubaliana mpaka Milioni 5. 

"Alinipa (Harmonize) Milioni 5 kwa ile shot. Which nilitaka Milioni 10 lakini akaniambia Gigy kwa nyimbo gani, nyimbo yenyewe lyrics video, shot yenyewe moja ya kwenye gari" alizungumza Gigy Money 

Gigy Money ni moja ya wasanii wanaofanya vizuri kwenye muziki nchini Tanzania akiwa na vibao kadhaa kama "Saubona" "Dharau" na nyinginezo nyingi.

Leave your comment