Producer S2kizzy Athibitisha Kufanya Ngoma Na Msanii Wa Nigeria, Patoranking

Image Source: Online 

Writer: Charles Maganga 

Bila shaka mtayarishaji wa muziki kutoka Tanzania S2kizzy yuko katika harakati za kupeleka sanaa yake duniani na hii ni baada ya producer kudokeza kufanya kazi mpya na msanii kutokea Nigeria Patoranking.

S2kizzy amedokeza kuhusu ujio wa project hiyo na Patoranking katika kipindi ambacho ngoma zake mbili ambazo ameziandaa yaani Daah ya Nandy na Mapoz ya Diamond Platnumz zinafanya vizuri.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, S2kizzy alipoat video akiwa na msanii Patoranking studio wakirekodi ngoma pamoja, jambo ambalo limepelekea mashabiki wengi kuwa na hamu ya kusikiliza collabo hiyo pindi itakapotoka.

S2kizzy ni mtayarishaji wa muziki kutokea Tanzania ambaye ngoma zake kama "Nitongoze" ya Rayvanny, "Komando" ya G Nako Na Diamond Platnumz, "Shisha" Ya Marioo na nyinginezo nyingi zimepelekea yeye kuwa moja ya watayarishaji wakubwa wa muziki Afrika.

Leave your comment