Country Wizzy Aandika Rekodi Mpya Nchini Tanzania Kwenye Mtandao Wa YouTube

Image Source: Online 

Writer: Charles Maganga 

Rapa kutokea Tanzania ambaye kwa sasa anatamba na ngoma yake ya kuitwa Way Back amefikisha idadi mpya ya wafuasi au subscribers kwenye akaunti yake YouTube.

Country Wizzy hivi karibuni amefikisha idadi ya subscribers laki mbili kwenye akaunti ya YouTube na hivyo kupelekea rapa huyo kuwa kwenye orodha ya wasanii wa Hip Hop nchini Tanzania wenye wafuasi wengi zaidi kwenye mtandao huo 

Kwa sasa Wizzy anashika namba 8 kwenye orodha ya rappers wenye subscribers wengi zaidi Tanzania baada ya Darassa, Nay Wa Mitego, Roma Mkatoliki, Dogo Janja, Professor Jay, Billnass na wengineo wengi.

Country alianzisha akaunti yake ya YouTube mwaka 2012 na mpaka sasa ana jumla ya views zaidi ya Milioni 10 kwenye akaunti yake ya YouTube.

Leave your comment