Exclusive DJ Mixes and 100% Ad-Free Music!
Ngoma Mpya Tanzania: Ali Kiba Aachilia ON FIRE
22 May 2023

Imange courtesy Instagram
Mwandishi Charles Maganga
Baada ya ukimya wa takriban miezi mitatu hatimaye “Only One King” kunako kiwanda cha Bongo Fleva, Ali Kiba ameachia mkwaju mpya kabisa wa kuitwa “On Fire”
“On Fire” inakuja siku chache kuelekea kwenye tamasha kubwa la kuitwa “Reloaded” ambapo Ali Kiba atatumbuiza kwenye jukwaa moja na msanii kutokea huko nchini Nigeria wa kuitwa Ayra Starr pale Superdome, Masaki.
“On Fire” ni ngoma kali ya Bongo Fleva ambayo ndani yake King Kiba anatoa sifa kedekede kwa mpenzi wake ambapo anamsifia mpenzi wake kutokana na urembo alionao. Kama kawaida, Ali Kiba ametumia sauti yake mujarab kupamba mkwaju huu.
“On Fire” ni ngoma ya tatu kutoka kwa Ali Kiba kwa mwaka huu baada ya hapo awali kuachia “Mahaba” ambayo imeshakusanya views takriban Milioni 9 kwenye mtandao wa Youtube na “Lalala” ambayo ameshirikiana na wasanii wa Kings Music.
Weekly Top 10 songs

Kamwambie3:47
chile-one-so-lucky4:02
Joy Is Coming3:08
TUMWAMBIE MUNGU ASANTE0:49
Malaika2:49
NALOKINGA2:52
Stima - Buruklyn Boyz5:04
Baddie remix feat Shannnon, aaronix, Tojo3:14
Buwooma2:44
Alifata Hela3:53
Top stories
- NEW MANAGEMENT
01 April
- Love
01 April
- My biography
02 April
- STREAM NEXARITO SONGS ON SPOTIFY
02 April


Leave your comment