Exclusive DJ Mixes and 100% Ad-Free Music!
Ngoma Mpya Tanzania: Ali Kiba Aachilia ON FIRE
22 May 2023

Imange courtesy Instagram
Mwandishi Charles Maganga
Baada ya ukimya wa takriban miezi mitatu hatimaye “Only One King” kunako kiwanda cha Bongo Fleva, Ali Kiba ameachia mkwaju mpya kabisa wa kuitwa “On Fire”
“On Fire” inakuja siku chache kuelekea kwenye tamasha kubwa la kuitwa “Reloaded” ambapo Ali Kiba atatumbuiza kwenye jukwaa moja na msanii kutokea huko nchini Nigeria wa kuitwa Ayra Starr pale Superdome, Masaki.
“On Fire” ni ngoma kali ya Bongo Fleva ambayo ndani yake King Kiba anatoa sifa kedekede kwa mpenzi wake ambapo anamsifia mpenzi wake kutokana na urembo alionao. Kama kawaida, Ali Kiba ametumia sauti yake mujarab kupamba mkwaju huu.
“On Fire” ni ngoma ya tatu kutoka kwa Ali Kiba kwa mwaka huu baada ya hapo awali kuachia “Mahaba” ambayo imeshakusanya views takriban Milioni 9 kwenye mtandao wa Youtube na “Lalala” ambayo ameshirikiana na wasanii wa Kings Music.
Weekly Top 10 songs

Trust No One3:13
chile-one-so-lucky4:02
Kamwambie3:47
Joy Is Coming3:08
Buwooma2:44
Udede Ft Msomali x Malume & Samas Alifata Hela Remix6:34
Msaliti 11:25
Leo3:39
Maringo4:00
NANI ft. Kamanda Pedeshee3:56
Top stories
- The Marathon
25 April


Leave your comment