Exclusive DJ Mixes and 100% Ad-Free Music!
Christina Shusho Aachia Albamu Ya “Hararat”
12 April 2023

[Picha: Instagram]
Mwandishi: Charles Maganga
Pata Habari za Muziki na Mixtapes Kwenye Telegram
Kwa takriban miezi minne na zaidi Christina Shusho amekuwa akidokeza kuhusu ujio wa albamu yake mpya na hivi karibuni malkia huyo wa muziki wa Injili nchini hatimaye ameachia albamu yake hiyo mpya ya kuitwa “Hararat”.
Ujio wa albamu ya “Hararat” ulisindikizwa na tamasha kubwa la uzinduzi lililopewa jina la “Mtoko Wa Pasaka” na katika uzinduzi huo, watu mbalimbali mashuhuri kama Diamond Platnumz, Mercy Masika kutokea Kenya, Rose Muhando, Ben Pol na wengineo wengi walipata kuhudhuria.
Albamu ya Hararat imemleta Christina Shusho mpya na ndani ya albamu hii yenye nyimbo 24, Shusho ameshirikisha wasanii tofauti tofauti kutokea Tanzania, Kenya, DRC Congo na Rwanda. Hii ni albamu ya kwanza kutoka kwa Christina Shusho ndani ya miaka 5.
Wasanii wengine wa Injili kutokea Tanzania walioachia miradi ya muziki hivi karibuni ni pamoja na Benjamin Weston pamoja na Gooduck Gozbert ambaye ameachia EP yake ya “Ushindi” hivi karibuni.
Weekly Top 10 songs

Kamwambie3:47
chile-one-so-lucky4:02
Joy Is Coming3:08
TUMWAMBIE MUNGU ASANTE0:49
Malaika2:49
NALOKINGA2:52
Stima - Buruklyn Boyz5:04
Baddie remix feat Shannnon, aaronix, Tojo3:14
Buwooma2:44
Alifata Hela3:53
Top stories
- STREAM NEXARITO SONGS ON SPOTIFY
02 April
- My biography
02 April
- Nobb challen
02 April


Leave your comment