Kusah Aturudisha Miaka Ya Nyuma Kwenye Ngoma Mpya "Wasi Wasi"

[Picha: Screengrab/YouTube]

Mwandishi: Charles Maganga

Pata Habari za Muziki na Mixtapes Kwenye Telegram

Msanii nguli kutokea nchini Tanzania, Kusah ameamua kukata kiu ya mashabiki zake kwa kuachia ngoma yake mpya inayokwenda kwa jina la Wasi Wasi.

Kama moja ya wasanii hodari sana ndani ya Bongo Fleva kwenye suala la uandishi wa nyimbo, Kusah ameendelea kutetea nafasi yake hiyo kupitia mkwaju wake mpya wa kuitwa Wasiwasi ambayo ni ngoma yake ya kwanza kwa mwaka 2023

Kwenye Wasi Wasi Kusah anachukua vionjo vya muziki wa zamani kutengeneza ngoma nzuri ambayo ndani yake anahadithia namna ambavyo hamuamini mpenzi wake huku akidokeza kuwa anaogopa sana kuachwa. Utapenda kila kitu kwenye ngoma hii kuanzia mashahiri yake matamu mpaka mdundo wake ambao unatukumbusha enzi za Msondo Ngoma na Bendi Ya Sikinde.

Cukie Dady ndiye amehusika kutayarisha ngoma hii. Ikumbukwe kuwa, Kusah na Cukie Dady ameshirikiana pia kutengeneza nyimbo kama Karibu, On Fire pamoja na I Wish.

https://www.youtube.com/watch?v=gBmgNzbknKM

Leave your comment