Nyimbo Mpya: Barnaba Classic 'Hadithi', Nandy 'Napona' na Nyimbo Zingine Zinazovuma Tanzania Wiki Hii

[Picha: Instagram]

Mwandishi: Charles Maganga

Pakua Ngoma Zake Mac Voice Bila Malipo Kwenye Mdundo

Bila shaka kama unafuatilia muziki kutoka nchini Tanzania, kufikia sasa utafahamu kuwa wiki hii kuna baadhi ya nyimbo ambazo zimeweza kufanya vizuri zaidi kwenye mtandao wa YouTube kutokana na mashabiki kupendelea kutazama au kusikiliza ngoma hizo kwenye mtandao huo.

Zifuatazo ni ngoma tano kutoka nchini Tanzania ambazo zinafanya vizuri sana kwenye mtandao wa YouTube :

Hadithi - Barnaba Classic Ft Diamond Platnumz

Ngoma namba 1 kwenye albamu ya, Barnaba Classic ya kuitwa "Love Sounds Different" imeendelea kufanya vizuri kwenye mtandao wa Youtube. Mashahiri mazuri pamoja na ushirikiano wa aina yake umesababisha ngoma hii kupendwa sana na mashabiki.

https://www.youtube.com/watch?v=-JaiCotheaU

Marry Me - Barnaba Classic Ft Marioo

Hii ni moja kati ya ngoma bora kwenye albamu ya Barnaba Classic hasa ukizingatia sauti nzuri ya Marioo ambayo inafungua ngoma hii pamoja na mashahiri mujarab ya Barnaba ambayo yanapamba sehemu ya pili ya ngoma hii.

https://www.youtube.com/watch?v=UIygyf9qa2U

Napona - Nandy Ft Oxlade

Wiki mbili tangu kuachiwa kwake, video ya Napona ya kwake Nandy akiwa na Oxlade imeendelea kufanya vizuri. Ukiweka kando video hii kuwa na stori nzuri lakini pia ubora wa picha pamoja na mitindo bora kabisa ya dansi imeweza kufanya video hii kuwa ya kipekee sana.

https://www.youtube.com/watch?v=73kHQmLaI9E

Fire - Zuchu

Zuchu ameendelea kukoleza umalkia wake kwenye muziki wa Tanzania kupitia video yake ya hivi karibuni ya kuitwa "Fire" ambayo imepokelewa kwa mikono miwili na mashabiki nchini na kufikia sasa imeshatazamwa mara Milioni 3.7 kwenye mtandao wa YouTube.

https://www.youtube.com/watch?v=78Zf-2wUh6c

Yanga - Marioo

Mashabiki wa timu ya Yanga wameendelea kumuunga mkono Marioo kupitia ngoma yake ya hivi karibuni ya kuitwa "Yanga" ambayo sio tu kwamba imeweza kuburudisha mashabiki wa Yanga pekee lakini kila mtu atakayesikiliza ngoma hii ataweza kukubali kipaji cha uandishi wa Marioo.

https://www.youtube.com/watch?v=6rWC2BGsDfs

Leave your comment