Exclusive DJ Mixes and 100% Ad-Free Music!
Nyimbo Mpya: Cheed Aachia ‘Ndoa’
28 January 2022

[Picha: YouTube]
Mwandishi: Charles Maganga
Pata Habari za Muziki na Mixtapes Bure Kwenye Telegram
Mwanamuziki kutokea nchini Tanzania Cheed ameachia ngoma mpya kabisa ambayo ameipa jina la ‘Ndoa’.
Wimbo huu unakuja takriban miezi mitatu tangu Cheed aachie ngoma yake ya mwisho ya kuitwa ‘Final’ ambayo pia iliweza kufanya vizuri sana kwenye mitaa mbalimbali hapa nchini Tanzania.
Soma Pia: Harmonize Amtaka Alikiba Kuburudisha Siku ya Kumposa Mpenzi Wake
Kwenye ‘Ndoa’, Cheed anaeleza namna ambavyo anampenda na kumhusudu sana mpenzi wake kiasi cha kutaka kufunga nae ndoa.
Cheed anatumia sauti yake nzuri kumhakikishia mpenzi wake kuwa hatomuacha na kutumia ujumbe kwa maadui zake kuwa hawataachana.
Ngoma hii ina maudhui ya kwenye harusi maudhui ambayo pia yanapatikana kwenye ngoma kama ‘Somo’ ya Kasim Mganga, ‘Iyena’ ya Diamond Platnumz na Rayvanny na ‘Nimwage’ ya Mrisho Mpoto na Harmonize.
Soma Pia: Nyimbo Mpya: Moni Centrozone Aachia EP Mpya ‘Road to Mazengo’
Ngoma hii imetayarishwa na Terriyo Monster ambaye pia amehusika kutayarisha ngoma ya Cheed ‘Final’ pamoja na ngoma ya Killy ‘Roho’.
Ngoma hii ni ya tatu kutoka kwa Cheed tangu ajiunge na Konde Gang, ngoma nyingine kutoka kwa Cheed tangu ajiunge na Konde Gang nyingine ni pamoja na ‘Wandia’ na ‘Final’.
Weekly Top 10 songs

Hatuachani8:47
Every push.2:01
Blessings Flow2:26
PENDEZESHA0:35
Daddy2:50
Bend and pouse2:54
Kisirani0:39
Boom party3:47
Nigina2:27
ONLY YOU JESUS5:44
Top stories
- Yopa freestyle
14 August
- Oxene Quiles feat kane gee
15 August
- Morning guys
16 August
- My new song is now out
14 August


Leave your comment