Moni Centrozone Afichua Mpango wa Country Boy Kufungua Lebo Yake

[Picha: Moni Centrozone Instagram]

Mwandishi: Brian Sikulu

Pata Habari za Muziki na Mixtapes Bure Kwenye Telegram

Mmoja kati ya marapa wakali nchini Tanzania Moni Centrozone amefichua mpango wa rafiki wake wa karibu Country Boy kufungua lebo yake.

Akizungumza katika mahojiano na kituo cha E FM, Centrozone alisema kuwa Country Boy yumo mbioni kufanikisha mipango yake kimuziki baada ya kuondoka lebo ya Konde Music Worldwide.

Soma Pia: Rapa Moni Centrozone Amsifia Zuchu kwa Ustadi Wake wa Kuimba Nyimbo za Mapenzi

Kwa mujibu wa Centrozone, alizungumza na Country Boy muda mfupi baada yake kuondoka Konde Gang. Alifichua zaidi kuwa Country Boy aliondoka lebo ya Konde Music Worldwide kwa amani.

Japo hakutoa habari zaidi, rapa huyo aliguzia tu kwa kifupi kuwa Country Boy kwa sasa anashughulikia kuanzisha lebo yake baada ya kufanya kazi na lebo tofauti.

“Nimekutana nae juzi alikuwa anashuti video yake, nafikiri yupo vizuri, yupo tayari kukutana na changamoto mpya baada ya kumaliza mkataba wake,nafikiri ana mipango ya kufungua label yake itakuwa kitu kizuri sana,” Centrozone alisema.

Soma Pia: Moni Centrozone Aeleza Sababu ya Kuandika Wimbo Wake ‘My Life’

Wawili hao wako na ukaribu sana kimuziki na kimaisha pia. Kumekuwa na furaha miongoni mwa mashabiki wao kuwa huenda wakashirikiana tena kimuziki haswaa baada ya Country Boy kukamilisha mkataba wake na Konde Music Worldwide.

Centrozone aliongezea kuwa amekuwa akifanya kazi na Country Boy japo hakubainisha iwapo kazi yoyote ipo njiani. Country Boy na Moni Centrozone ni miongoni mwa marapa waliokubalika katika muziki wa kizazi kipya Tanzania.

Leave your comment