Exclusive DJ Mixes and 100% Ad-Free Music!
Mkubwa Fella Azungumzia Tetesi za Uhasama Kati ya Mbosso na Aslay
3 November 2021

[Picha: The Standard]
Mwandishi: Charles Maganga
Pata Habari za Muziki na Mixtapes Bure Kwenye Telegram
Aliyekuwa meneja wa kundi la Yamoto Band Mkubwa Fella amezungumza kwa undani kuhusu tetesi zilizosambaa kwa muda mrefu kuwa Mbosso na Aslay hawana maelewano mazuri.
Akiongea kwenye kipindi cha The Switch, Mkubwa Fella ambaye ni kama mlezi wa wasanii hao alisema kuwa kwa upande wake haoni kama kuna mgogoro wowote baina ya wasanii hao.
Soma Pia: Aslay vs Marioo: Nani Bora Zaidi katika mziki wa RnB?
Kwa mujibu wa Mkubwa Fella, mashabiki ndio huwashindanisha wasanii hao wawili.
"Ukiona hivyo kuna mashabiki tu wanaingia tu kwenye midomo midomo lakini mi naamini wale wote ni ndugu na wamezaliwa kwenye koo moja. Kwa sababu mwisho wa siku sasa hivi Mbosso ana management yake alafu ukiangalia na Aslay ana management yake lakini mwisho wa siku wao wafanye kazi mambo yaende," alizungumza Mkubwa Fella.
Soma Pia: Mkubwa Fella Azungumzia Kuvunjika kwa Yamoto Band, Ukimya wa Aslay
Mkubwa Fella ambaye pia ni mmojawapo ya wasimamizi wa kimuziki wa mwanamuziki Diamond Platnumz aliwahasa wasanii hao yaani Aslay pamoja na Mbosso waendelee kufanya kazi na ikibidi watoe ngoma ya pamoja.
"Kuna siku wakae na wenyewe waangalie wafanye kitu kimoja kwa pamoja ukiangalia Beka yuko smart ukiangalia na Enock yuko smart wao nao wawe masmart wawili wafanye kitu cha pamoja inatosha," alimalizia Mkubwa Fella.
Kundi la Yamoto lilikuwa maarufu sana nchini Tanzania kuanzia mwaka 2013 hadi 2017 ambapo lilivunjika.
Weekly Top 10 songs

CHAMPION GAL3:00
Tudo Trocado3:17
ONLY YOU JESUS5:44
Joy Is Coming3:08
Akaana kokukyalo2:21
Nasema3:02
BESTIE2:26
Minha Historia3:41
Baraka4:33
Mikono Juu2:49
Top stories
- Listen To Me Please
04 July
- Baamane
04 July
- About luckystarzs
05 July
- KVM PRO UG new music
04 July


Leave your comment