Busta Rhymes Amsifu Diamond, Amtaja Kuwa Michael Jackson wa Afrika

[Picha: Diamond Instagram]

Mwandishi: Brian Sikulu

Pata Habari za Muziki na Mixtapes Bure Kwenye Telegram

Mwanamuziki wa Tanzania Diamond Platnumz amesifiwa na mwimbaji wa Amerika Busta Rhymes kwa kuwa Michael Jackson wa Afrika.

Michael Jackson anakumbukwa kwa kuwa mfalme wa muziki wa Pop. Alikuwa mmoja wa mwanamuziki wa kimataifa aliyefanikiwa zaidi na alikuwa na mashabiki wengi duniani.

Busta Rhymes alitoa taarifa hiyo wakati alipokutana na Diamond Platnumz huko Marekani.

Soma Pia: Nyimbo Mpya: Diamond Platnumz Aachia Wimbo Mpya ‘Kamata’

Kulinganishwa kwa Diamond na Michael Jackson kuna maana kwake kama msanii. Inaonyesha kwamba amekua na kufikia kiwango cha kimataifa.

Busta Rhymes ambaye alimsifu Diamond pia ni msanii anayeheshimika katika tasnia ya burudani ya kimataifa. Maoni yake kuhusu Diamond kwa hivyo inachukuliwa na uzito mwingi. Ulinganisho huo pia umeibua hisia tofauti kati ya mashabiki. Wengi wamejiunga kumsifu Diamond wakitaja kuwa alistahili kutambuliwa kama msanii wa kimataifa.

Soma Pia: BET Awards: Burna Boy Amshinda Diamond, Aibuka Mshindi wa Best International Act

Kwa sasa, Diamond yuko Marekani ambapo anamalizia albamu yake akisaidiwa na wadau wengine wa kimataifa katika tasnia ya muziki.

Diamond pia alisafiri kwenda Marekani kuhudhuria hafla ya tuzo za BET ambapo alikuwa ameteuliwa katika kitengo cha Best International Act. Diamond alishindwa kwenye kitengo hicho na Burna Boy.

Wasanii na watu mashuhuri Tanzania na Afrika mashariki wamejitokeza na kumsifu Diamond licha ya kupoteza kwenye tuzo hiyo.

Leave your comment