Exclusive DJ Mixes and 100% Ad-Free Music!
Ibraah Ampongeza Diamond Platnumz Kwa Uteuzi wa BET
2 June 2021

[Picha: AllAfrica]
Mwandishi: Brian Sikulu
Pata Habari za Muziki na Mixtapes Bure Kwenye Telegram
Mwanamuziki Ibraah kutoka Konde Music Worldwide amewashangaza mashabiki wake baada ya kutangaza wazi kumuunga mkono Diamond katika Tuzo zijazo za BET.
Diamond aligonga vichwa vya habari baada ya kuteuliwa kwa kitengo cha Best International Act kwenye Tuzo za BET.
Soma Pia: Nyimbo Mpya: Ibraah Aachia Video Mpya ‘Mapenzi’
Idadi kubwa ya watu mashuhuri haswa wanamuziki walijitokeza kumpongeza Diamond. Hata hivyo, Mkurugenzi mkuu wa Konde Music Harmonize hakumtambua Diamond Platnumz kwa mafanikio hayo kutokana na ushindani wao wa muda mrefu.
Awali wawili hao walikuwa marafiki wazuri na Harmonize alipata umaarufu kupitia lebo ya Diamond ya WCB. Waligawana njia baada ya kutokubaliana mara kwa mara.
Soma Pia: Rais Samia Suluhu Ashauri Serikali yake Kuzingatia Changamato za Wasanii
Harmonize aliondoka na kuzindua Konde Gang. Ni chini ya Konde Gang ambapo Ibraah alisainiwa na akaachia wimbo uliomwongoza kufanikiwa.
Akizungumza wakati wa mahojiano ya hivi karibuni, Ibraah aliibuka na kukiri uteuzi wa Diamond akitaja kwamba ameifanya Tanzania kujivunia.
Aliendelea kumtakia mafanikio na ushindi katika tuzo hizo. "Diamond ni msanii mkubwa. Ukizungumzia wasanii wakubwa wa Tanzania lazima umtaje Diamond. Mimi naona ni baraka sababu sio mara ya kwanza yeye kuingia katika hizo tuzo, na mwenyezi Mungu amfanyie wepesi arudi na tuzo nyumbani," Ibraah alisema wakati wa mahojiano.
Weekly Top 10 songs

KAPEKE LONDON2:23
BIkola2:58
In My Bed2:50
Buwooma2:44
Ex Nkubilako ft DonMusa2:55
Baddie remix feat Shannnon, aaronix, Tojo3:14
CHAMPION GAL3:00
Paver2:55
Nitampeleka kwa Mama (ft. Xouh)3:44
Joy Is Coming3:08
Top stories
- NEW SONG ALERT
16 May
- Generation
16 May
- Boom Shakatah means
17 May
- Date of birth
15 May


Leave your comment