Nyimbo Mpya: Ngoma 5 Mpya Zinazovuma Bongo Wiki Hii [Video]
26 May 2021
[Picha: Instagram]
Mwandishi: Omondi Otieno
Pata Habari za Muziki na Mixtapes Bure Kwenye Telegram
Wasanii wa Bongo Fleva wanaendelea kuonyesha umahiri wao eneo la Afrika Mashariki kwakuachia ngoma mpya zinazotamba.
Wiki hii, wasanii kadhaa wameachia nyimbo mpya. Katika nakala hii, tunaangazia ngoma zinazotambaa kwenye mtandao wa YouTube Tanzania:
Soma Pia: Rayvanny Atajwa Msanii wa Pili Bongo Mwenye Mauzo Makubwa ya Muziki
Rostam ft Ferooz - Hujambo Mwanangu
Kwenye wimbo huu, Rostam wamemshirikisha msanii mwenzao maarufu Ferooz. Katika mistari yao, wanaangazia kazi aliyofanya hayati rais John Pombe Magufuli na rais wa sasa Samia Suluhu. Kufikia sasa wimbo huu una watazamaji zaidi ya laki nne.
Do Lemme - Go MC Kinata ft Ibraah
Huu ni wimbo wa Singeli wake MC Kinata ambao alimshikisha Ibrah kutoka Konde Music Worldwide. Kwenye mistari yao Kinata, anaimba kuhusu upendo huku Ibraah akitupa michambo. Kufikia sasa ni wimbo ulio na watazamaji zaidi ya laki tano kwenye YouTube.
Kelebe – Rayvanny ft Innoss’B
Hii ni moja ya nyimbo zilizo kwenye alabamu yake Rayvvany ‘Sounds From Africa’. Wimbo huu umepokelewa vizuri huku wafuasi wakitengeza video fupi wakijitumbuiza na wimbo huu.
Nobody - Anjella
Hii ni kazi yake Anjella kutoka Konde Gang iliyopokelewa kwa ukubwa sana. ‘Nobody’ ni wimbo wa mapenzi na kufikia sasa una watazamaji zaidi ya milioni mbili kwneye mtandao wa YouTube.
Kiss Me – Mbosso
Huu ni wimbo wa mapenzi kutoka albamu ya Mbosso ‘Definition of Love’. Kwenye ngoma hii, ushairi wa Mbosso unajitokeza huku akisihi mpenzi wake ambusu.
Leave your comment