TMK Warejea! Juma Nature Amshirikisha Chege Kwenye Wimbo mpya ‘Kucha’ [Video]

[Picha: Juma Nature Instagram]

Mwandishi: Branice Nafula

Pata Habari za Muziki na Mixtapes Bure Kwenye Telegram

Nguli wa mziki wa Hip-hop Juma Nature ameachia wimbo mpya kwa jina ‘Kucha’ akimshirikisha aliyekuwa katika kundi lake TMK Wanume Halisi Chege Chigunda.

‘Kucha’ ni wimbo ambao wawili hawa wanamsifia binti ambaye wamependezwa naye. Ukiskiliza na kuitazama kanda ya wimbo huu, ufundi na ushairi wa wasanii hawa unadhihirika.

Soma Pia: Nyimbo Mpya: Ngoma 5 Zilizoachiwa Bongo Wikendi Iliyopita [Video]

Juma Nature anaanza kwa kusifia uno la mrembo mmoja ambaye kulingana naye ni binti halisi kwani ni dada amelelewa kipwani. Vile vile anasafia jinsi alivyo na maumbile ya kuvutia.

“Hataki hataki watoto wadogo watampa nini huyo?? Ni pin kali huyo!! mkamate huyo!!” aliimba Nature.

Pia kupitia sweta alilovaa Nature kwenye kanda hii ametangaza kuwa kundi la wanamziki wa hip-hop TMK wamerejea.

Soma Pia: Wasifu wa Maua Sama, Nyimbo zake Bora, Mahusiano na Thamani Yake

Sweta hiyo alisoma ‘TMK is Back’. Chege kwa upande wake aliingia na mistari yake ya kifundi alipoendelea kumsifia binti huyo mrembo.

Kanda ya wimbo huu ilifanywa kwa ustadi mkubwa na mwelekezaji Joma wa Tanzania na ilitengezwa mjini Dar es Salaam.

Wakati mashabaki wanaendelea kuupokea wimbo huu kwa kishindo, ni muhimu kukumbuka kuwa Juma Nature ni msanii mojawapo aliyepeperusha mziki wa Tanzania kwa ustadi mkubwa miaka ya nyuma.

Anaporejea kwenye ulingo wa mziki heshima na hadhi yake itabaki kusifiwa. Kwa sasa wimbo ‘Kucha’ una watazamaji zaidi ya laki moja.

v=xLJHc4DDfts&ab_channel=ChegeChigundaChegeChigundaOfficialArtistChannel

Leave your comment