Exclusive DJ Mixes and 100% Ad-Free Music!
Hamisa Mobetto Kuachia Ngoma Mpya Hivi Karibuni
13 October 2020

[Photo Credit:Hamisa Mobetto Instagram]
By Branice Nafula
Msanii kutoka Tanzania Hamisa Mobetto ametangaza kwamba hivi karibuni ataachia ngoma yake mpya.
Hii ni baada ya kutoachia mziki sasa kwa muda wa karibu mwaka mmoja.
Kwa sasa haijulikani ni lini wimbo huu utazinduliwa na inakisiwa kuwa Hamissa atamshirikisha msanii kutoka Nigeria.
Kwa upande wake Hamissa alitangaza hili kupitia mtandao wa Instagram na kuandika haya: “Guess who ….?Subscribe to my YouTube Channel (Hamisa Mobetto) Or you can just click the Link on My Bio…”

Kufikia sasa mashabiki wa Hamisa Mobetto wanaamini kuwa anayeshirikishwa kwa wimbo huo ni msanii kutoka Nigeria aitwaye Singah.
Singah ni mwanamziki anayejulikana kwa kufanya wimbo “Teyamo” uliompa nafasi ya kujilikana barani Afrika.
Miezi kadha iliypota, Hamisa alizindua tetesi baada ya kushirikishwa na Alikiba katika wimbo wake wa ‘Dodo’.
Katika ‘Dodo’ Hamisa alicheza sehemu ya mpenzi wa Alikiba ambapa walifanya harusi. Video ile ilileta tetesi sana wengi wakimkera Hamisa kwa kukubali kushirikishwa ilhali yeye na Diamons wana motto pamoja, na Diamond na Alikiba hawana uhusioano mzuri.
Weekly Top 10 songs
Top stories
- The Marathon
25 April
- TRUE LOVE
26 April
- HOWE WOU KUMA
25 April
- O Daynor pisom 03 casou
24 April




Leave your comment