Exclusive DJ Mixes and 100% Ad-Free Music!
TANZANIA: Alikiba Afunguka Sababu ya Kufuta Wimbo
9 October 2018

Msanii wa muziki wa bongo fleva Alikiba ambaye hivi karibuni amekumbana na lawama na kejeli za mashabiki baada ya kufuta wimbo wake mpya wa 'hela', amefunguka sababu za kufuta wimbo huo uliomuweka pabaya.
Akizungumza na kwenye Planet Bongo ya East Africa Radio, Alikiba amesema sababu kubwa ya kufuta wimbo huo ni siku ambayo aliachia, kwani haikuwa siku ambayo huitumia kuachia nyimbo mpya.
“Siku yenyewe haikuwa siku yangu ambayo napenda kurelease nyimbo, ilikuwa siku ya Jumanne so tukamwambia jamaa autoe, inatakiwa siku kama ya leo Alhamisi, ndio maana ulikuta umetoka kwenye Youtube, ila sasa hivi ukiingia utaikuta”, amesema Alikiba.
Alikiba amelazimika kutoa maelezo hayo baada ya kushambuliwa na mashabiki kuwa ameutoa wimbo huo kwa kuwa ni mbaya na wa zamani.
Source: eatv.tv
Weekly Top 10 songs

In My Bed2:50
KAPEKE LONDON2:23
BIkola2:58
Buwooma2:44
Baddie remix feat Shannnon, aaronix, Tojo3:14
Paver2:55
Nitampeleka kwa Mama (ft. Xouh)3:44
Ex Nkubilako ft DonMusa2:55
CHAMPION GAL3:00
Kamwambie3:47
Top stories
- UPCOMING EP FROM EMKAY64
14 May
- Daniel Sifuna
14 May
- Generation
16 May
- NEW SONG ALERT
16 May


Leave your comment