Exclusive DJ Mixes and 100% Ad-Free Music!
TANZANIA: Nafunga Ndoa Na Mtu Nimpendae - Billnass
14 June 2018

Msanii wa muziki nchini Billnass, amedai kuwa anampango wa kufunga ndoa na mpenzi wake wa sasa itakapofika mwakani kwasababu anapenda maisha ya ndoa nakuwa na familia kwani ni kitu muhimu kwake.
Msanii huyo amesema hayo leo Juni 11, 2018 na kuongeza kuwa hatua ya kuingia katika ndoa inatokana na uamuzi wake mwenyewe na wala sio kusukumwa na watu au matukio aliyopitia katika maisha yake ikiwemo kufuta skendo ya video baina yake na msanii Nandy.
“Mimi nikiingia katika ndoa sio kwasababu ya kufuta skendo, naoa kwasababu naingia kwenye maisha ambayo nayapenda, familia kwangu ni kitu muhimu sana lakini pia naingia katika ndoa na mtu ambaye nampenda zaidi, ndoa ni mipango ya Mungu lakini kwa ratiba zangu nilikuwa natamani mwakani nioe” amesema Billnass.
Billnass aliongeza kuwa mpenzi wake wa sasa ndiye aliyekuwa mtu wa kwanza kumuunga mkono wakati wa kipindi kigumu alichopitia baada kusambaa kwa video yake na Nandy, amesema “Sijaachana na mpenzi wangu nipo nae mpaka sasa ni mtu mwenye akili na ndiyo mtu pekee niliyekuwa nawasiliana nae sana na kunifariji ni mtu anayejielewa”
Kwa upande mwingine msanii huyo amedai kwamba kusambaa kwa video yake na msanii wa kike Nandy lilikuwa ni jambo baya na alifanya makosa kwani lengo lake kama msanii, watu wamjue kupitia kazi zake na sio mambo ambayo yanaharibu taswira yake ya usanii.
Source: eatv.tv
Weekly Top 10 songs

In My Bed2:50
KAPEKE LONDON2:23
BIkola2:58
Buwooma2:44
Baddie remix feat Shannnon, aaronix, Tojo3:14
Paver2:55
Nitampeleka kwa Mama (ft. Xouh)3:44
Ex Nkubilako ft DonMusa2:55
CHAMPION GAL3:00
Kamwambie3:47
Top stories
- UPCOMING EP FROM EMKAY64
14 May
- Daniel Sifuna
14 May
- Generation
16 May
- NEW SONG ALERT
16 May


Leave your comment