TANZANIA: “Naachia Ngoma Moto” Shilole Awaahidi Mashabiki

Zuwena Mohammed anayetambulika sana kama Shilole anafuraha mingi baada ya kukamilika kwa Mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani.

Hii inamtia msanii huyu furaha kwa sababu sasa anauwezo wa kuachia kazi zake mpya, kitu ambacho hangekifanya hapo awali kwa sababu ya kuhufadhi sheria za dini yake.

Akizungumza kwenye mahojiano,Shilole alisema kuwa ilimbidi kukaa kimya lakini kwa sasa akona mipango ya kuiachia kazi kubwa kubwa hivi karibuni, hivyo akiwaonya wanamuziki wenzake kujipanga.

Shilole alisema…

“Wanamuziki wajipange maana nina ngoma kali itakayotoka hivi karibuni, ikiwa ni baada ya kukaa kimya kwa muda kutokana na mwezi mtukufu, lakini kwa sasa umeisha hivyo nakuja kwa kasi ya ajabu."

Source: ghafla.com

Leave your comment