TANZANIA: Linah asema kwa sasa hayupo tayari kumuweka wazi mpenzi wake

 

 

Msanii Linah Sanga ambaye kwa sasa anafanya vizuri na ngoma yake ya 'Imani' amefunguka na kusema kuwa kwa mambo ambayo tayari yamemkuta kwenye mahusiano hayupo tayari tena kumuweka wazi mpenzi wake kwenye mitandao ya kijamii.

Linah Sanga akiongea kwenye kipindi cha Enews amesema kwamba kwa sasa yeye hayupo tayari kumuweka wazi mpenzi wake kama ilivyokuwa awali kwani jambo hilo kwanza linapelekea watu kuanza kufuatilia maisha yake ya mahusiano na si kazi zake za muziki.

Mbali na hilo Linah Sanga amefunguka na kusema kuwa wapo watu kwenye mahusiano wanaingia ili kutaka kuonja penzi la mtu na kuona huyo mtu yupoje kwenye mapenzi ila hawana mipango endelevu wala hawaangalii mipango ya baadaye.

 

Pakua app ya Mdundo sasa: smarturl.it/mdundo_ig_play_tz

 

 

Leave your comment

Top stories