Exclusive DJ Mixes and 100% Ad-Free Music!
TANZANIA: Diamond hajawahi kutoka na mama mtoto wangu - Shetta
6 May 2016

Shetta amekanusha taarifa zilizozagaa mitandaoni kuwa Diamond amewahi kutoka kimapenzi na mama Qayllah.
Wiki kadhaa zilizopita Shetta alifuta picha zote kwenye akaunti yake ya instagram huku akiwaacha mashabiki wake wakijiuliza maswali mengi kutokana na kitendo hicho.
Akiongea kwenye kipindi cha Leo Tena, kinachoruka kupitia Clouds FM, Shetta amesema, “kuhusu suala la mama Qayllah kutoka na Diamond hakuna ukweli wowote.”
“Kuhusu suala la kufuta picha ni management yangu mpya ilinishauri hivyo ndiyo maana unaona nilifuta picha zote hizo. Team team tu wameanzisha na kuzisambaza mitandaoni lakini hakuna ukweli wowote namuamini sana mke wangu. Mimi na Diamond tuko vizuri ila hizo,” aliongeza.
Chanzo: Bongo5
Weekly Top 10 songs
Top stories
- New song
13 April
- Inspirational
13 April




Leave your comment