Exclusive DJ Mixes and 100% Ad-Free Music!
TANZANIA: Aika aelezea sababu ya yeye na Nahreel kutoka kwenye kundi la Pah one
25 April 2016

Kabla ya kundi la Navy Kenzo kuwepo, walikuwa katika kundi liitwalo Pah One lakini walikuja kutengana na kuunda kundi lao liitwalo Navy Kenzo.
Katika mahojiano ya Aika na Mdundo.comalielezea sababu zilizpelekea mpka wakatoka kwenye kundi hilo la Pah One.
“Hakukuwa na maelewano kati ya pande mbili, wawili walikuwa ni ndugu na kwa upande mwengine mimi na Nahreel tulikuwa tunadate lakini hata hivyo haikuwa ndio sababu ya sisi kutengana. Sababu kubwa ni kwamba tulikuwa tunatofautiana katika fikra zetu upande wangu na Nahreel pamoja na upande wao.”

“Walikuwa wanasema wao ndio mastaa kuliko sisi na wao ndio waliokuwa wanamchango kubwa kwenye muziki.” Aliongeza Aika. Aika na Nahreel hawakukata tamaa katika muziki na wakazidi kupambana.
Aliendelea Aika na kusema, “Tukatoa nyimbo mimi na Naheel inaitwa “Usinibwage”. Kwakuwa tumekuwa pamoja tangu mwaka 2008 hatujawahi kuwa na tatizo kwahiyo tukaona kwanini tukate tamaa, tukaona tuform a group na tuendeleze muziki ambao tulikuwa tumeuanzisha. Tukaja na jina la Navy Kenzo, Kenzo ikiwa na maana watu shupavu,wanyenyekevu na Army kama inavyojulikana ni wanajeshi, kwahiyo tukaona tujiite Navy Kenzo”
Kwasasa kundi la Navy Kenzo linaendelea na tour yao iitwayo Kamatia Tour, Lights Up Tour ambayo wameenda maeneo tofauti kama Dodoma, Morogoro, Iringa na Nairobi.
Weekly Top 10 songs

Kamwambie3:47
chile-one-so-lucky4:02
Buwooma2:44
Joy Is Coming3:08
Nakupenda3:12
Udede Ft Msomali x Malume & Samas Alifata Hela Remix6:34
Msaliti 11:25
Paver2:55
Ssirivawo ft yven feiz2:10
Ziyakuba kabotu6:57
Top stories
- #NEW MUSIC #NEW artist #RAYMATS!
30 April
- BABA FELA
30 April
- Nordman--Kelly yo collabo
30 April


Leave your comment