Exclusive DJ Mixes and 100% Ad-Free Music!
TANZANIA: Nataka nimuoe Vanessa ndoa kabisa - Bright
21 April 2016

Msanii chipikizi wa nchini, Bright anasema ana ndoto kubwa ya kumuoa diva huyo ambaye ni mwandani wa msanii Jux, huku akiweka wazi kuwa Jux hamuogopi kwani hajamuoa.
“Nampenda sana natamani kumuoa ndoa kabisa, unajua msicheke ni kitu ambacho naongea niko serious kabisa, natamani kumuoa kabisaa, ni mwanamke mzuri mwenye mvuto, mwanaume yoyote aliyekamilika lazima atamani”, alisema Bright.
Mtangazaji wa kipindi hiko Dulla alipomuuliza kuhusu itakuwaje iwapo Jux akijua, alijibu kwa kujiamini kuwa hana wasi wasi kwani Jux hajamuoa Vanessa, na yeye anataka kumuoa kabisa awe mke wake wa ndoa,
“Niko kwenye process hata kama Jux yupo naye, hawajaoana nina nafasi ya kumwambia nikamvisha pete ndoa kabisa, na sio namsubiri amuache, naweza nikamnyang'anya braza, mpaka sasa hakuna aliyetangaza ndoa kwa V Money”, alisema Bright.
Pamoja na hayo yote Bright amesema wimbo huo anau-dedicate kwa Vanessa, akimtaka amtunzie ili amuoe, huku akiwataka mashabiki kumuunga mkono kwa kuomba nyimbo yake ipigwe kwenye radio.
Weekly Top 10 songs

Kamwambie3:47
chile-one-so-lucky4:02
Buwooma2:44
Joy Is Coming3:08
Nakupenda3:12
Udede Ft Msomali x Malume & Samas Alifata Hela Remix6:34
Msaliti 11:25
Paver2:55
Ssirivawo ft yven feiz2:10
Ziyakuba kabotu6:57
Top stories
- #NEW MUSIC #NEW artist #RAYMATS!
30 April
- Nordman--Kelly yo collabo
30 April
- One and only
01 May


Leave your comment