Exclusive DJ Mixes and 100% Ad-Free Music!
TANZANIA: Sijawahi kuendesha gari ya mtu – Baraka Da Prince
20 April 2016

Msanii wa muziki wa bongo fleva Baraka Da Prince amejikuta akipatwa na tetesi ya kwamba magari anayotumia si ya kwake na kuwa anagongea kwa marafiki.
Akipiga stori na eNewz Baraka amekanusha kashfa hizo na kusema kuwa wanaosema anagongea magari ni machizi tu. Zaidi Baraka ameongeza kuwa yeye anamiliki magari zaidi ya moja na hajawahi kuendesha gari ya mtu.

Pia Baraka hakuficha kuwa kwa sasa amekwisha mtambulisha msanii mwenzake Naj kwa wazazi wake kuwa ndiye mchumba wake, na amemvisha pete ya ahadi kuwa atakuwa naye milele daima. Alipoulizwa kuwa pete hiyo inamaanisha ana nia ya kumuoa Naj, Baraka alisema “Kwa hilo Mungu ndiye anayejua”.
Weekly Top 10 songs

Black Mark utandilubi omwami wangu5:21
KAPEKE LONDON2:23
In My Bed2:50
Paver2:55
CHAMPION GAL3:00
Ex Nkubilako ft DonMusa2:55
BIkola2:58
The Prelude of Grace1:31
Joy Is Coming3:08
Worship My King5:00


Leave your comment