Exclusive DJ Mixes and 100% Ad-Free Music!
TANZANIA: Ruby asingekuwa na management tungemchukua – Babu Tale
17 March 2016

Meneja wa msanii mahiri wa msanii Diamond Plutnumz maarufu kama Babu Tale amefunguka kuhusu projects mbalimbali za lebo ya WCB na kueleza wamejipanga kuibua vipaji vipya bila kubagua jinsia na kusajili wasanii wakubwa kwenye lebo hiyo ili kupanua wigo wa kibiashara na tasnia ya muziki.

Ruby
Akizungumza suala la kuibua vipaji bila kubagua jinsia meneja huyo ameeleza kuwa wanahitaji kuibua vipaji vya wanawake kwasababu kuna wanawake wachache wanaotamba kwenye ramani ya muziki, hivyo wanahitaji msanii wa kike mwenye uwezo kama wa Rubby au zaidi ya hapo, huku akieleza kuwa Rubby angekuwa hana menejimenti wangemchukua kwenye lebo ya WCB.

Rich Mavoko
Kuhusu suala la uvumi wa msanii Rich Mavoko kuhamia kwenye lebo ya WCB Babu Tale ameeleza kuwa utakapo fika wakati muafaka uongozi wa WCB utaeleza kuhusu ujio wa msanii huyo mwenye sauti ya kuvutia.
Weekly Top 10 songs
Top stories
- One and only
01 May
- SHUKRANI
02 May
- Okello oyumu
01 May




Leave your comment