TANZANIA: Mambo 11 yawezekana huenda ulikua hujui kuhusu Shaa

Kuna mambo 11 yawezekana ulikua hujui kuhusu Shaa, kupitia kipindi cha Chill n Sky unaweza kupata mambo 11 yanayomuhusu Shaa.

  1. Alizaliwa mwaka 1985
  2. Mtoto wa mwisho kwenye familia ya watoto wanne
  3. Baba yake ni mzaliwa wa Kyela, mama yake ni mzaliwa wa Nachingwea.
  4. Anatoka kwenye familia ya kimuziki, kaka yake ni mwanamuziki wa reggae, dada yake Nelly Kaisi ni mpiga gitaa la base.
  5. Baba yake, Dr Kaisi (amestaafu mwaka 2015) ni binwa wa magonjwa ya wanawake Tanzania. Alikuwa akiwatibu wake wa maraisi Tanzania.
  6. Mama yake alikua Kabidhi Wasii Mkuu wa Serikali wa kwanza mwanamke.
  7. Akiwa amemaliza kidato cha nne hakuwa amepanga kushiriki katika Coca Cola Popstars, alimsindikiza rafiki yake (Zubeda) ambaye hakutokea. Wakati anasubiri wahusika walimwambia aimbe tu lakini akaonyesha maajabu na akachaguliwa. Top 6 wallinia yeye, Langa, Witness, Illu, Terrence na Enika.
  8. Alipata Scholarship na kwenda kusoma Sanaa (Art & Design) Washington DC, Marekani. Ni mchoraji wa picha. “Nachora kila kitu”.
  9. Jina lake Shaa alipewa na marehemu Ngwair. Jina Shaa lilitoka kwenye jina (WAKILISHA) aliongeza A mwishoni na kuwa Shaa.
  10. Alikuwa msanii wa kwanza wa kike kusainiwa kwenye lebo ya Mj Records.
  11. Mwanzoni Master J alikuwa akimchana na kuhisi hakustahili kushinda mashindano ya Popstars. Anasema hiyo ilimjenga na kumtengeneza kuwa msanii mzuri.

 

Unaweza kusikiliza mahojiano yote ya Shaa katika kipindi cha Chill n Sky hapa:

 

 

 

Chanzo: Bongo5.com

 

Leave your comment