Exclusive DJ Mixes and 100% Ad-Free Music!
TANZANIA: Manager wa Diamond asema Rich Mavoko hajasign WCB
11 March 2016

Kumekuwepo na taarifa kwamba msanii wa bongofleva Rich Mavoco amechukuliwa na sasa kazi zake zitakua zinasimamiwa na lebo ya Diamond Platnumz ‘WCB’ na aliyenukuliwa akisema hivyo ni Harmonize ambaye ni msanii wa WCB.

Jorge Mendez 'Sallam SK' akiwa na Diamond Platnumz
Hata hivyo Diamond Platnumz kwenye Exclusive Interview na OnAIR with Millard Ayo wiki kadhaa zilizopita alisema miongoni mwa mipango mikubwa aliyokuwa nayo ilikua ni kumsaini Rich Mavoko kwenye lebo ya WCB ila bado mipango ilikua haijakamilika.
Sasa baada ya stori za leo kutoka kwamba imethibitishwa Mavoko kasainiwa WBC, meneja wa Diamond Platnumz Sallam alichukua time yake kumjibu mmoja wa watu waliomuandikia kwenye Twitter na kusema ‘Mavoko hajasainiwa WCB bado, ila Harmonize ameona kuwa Rich alikuwa na mazungumzo na viongozi akajua ni tayari. ukweli ni kwamba haja sign’

Rich Mavoko
Weekly Top 10 songs

Black Mark utandilubi omwami wangu5:21
KAPEKE LONDON2:23
In My Bed2:50
Paver2:55
CHAMPION GAL3:00
Ex Nkubilako ft DonMusa2:55
BIkola2:58
The Prelude of Grace1:31
Joy Is Coming3:08
Worship My King5:00
Top stories
- Excellent Jesus
26 May
- Trending song
24 May
- ICE PRINCESS SONGS
24 May


Leave your comment