Exclusive DJ Mixes and 100% Ad-Free Music!
TANZANIA: Baba wa Diamond ajipanga kumuona Mjukuu wake Tiffah kwa mara ya kwanza
29 February 2016

Hatimaye baba wa msanii gwiji anayetamba Afrika wa miondoko ya Bongo Fleva, Diamond Platnumz ameruhusiwa kumuona mjukuu wake Tiffah.
Ni baada ya mvutano wa huku na huku kutokana na tofauti zao, kwa sasa wawili hao wamemaliza tofauti zao na kumfanya mzee Abdul Juma kuwa na sababu ya kufurahi tena.
Kwa mujibu wa Global Publisher, wamesema Diamond amemsamehe baba yake na kumruhusu kuweza kumuona mama mtoto wake (Zari) na mjukuu wake Tiffah.
“Baba Diamond hana kinyongo wameshazungumza na mama Diamond wameshamaliza tofauti zao, Diamond mwenyewe hana tatizo kilichobaki ni kwenda tu kule kufanya dua”, kilisema chanzo cha Global Publisher.
Diamond na mzee wake hawakuwa na maelewano baada ya kuwatelekeza mama yake na ndugu zake katika umri mdogo kutokana na mambo ya kifamilia.
Weekly Top 10 songs

Black Mark utandilubi omwami wangu5:21
KAPEKE LONDON2:23
In My Bed2:50
Paver2:55
CHAMPION GAL3:00
Ex Nkubilako ft DonMusa2:55
BIkola2:58
The Prelude of Grace1:31
Joy Is Coming3:08
Worship My King5:00


Leave your comment