Exclusive DJ Mixes and 100% Ad-Free Music!
TANZANIA: Jay Mo naye aongelea kuhusu suala la kufanya video nje ya nchi.
29 February 2016

Baada ya hivi karibuni msanii wa muziki ya miondoko ya hiphop wa nchini Kenya Prezzo kuwaambia wasanii wa Tanzania wanaendea kufanya video ya nchini hususani nchini Afrika Kusini na kuwaasa kubaki nchini mwao ili kukuza soko la ndani la muziki.
Pia msanii mahiri wa miondoko ya hiphop wa nchini Tanzania Jay Mo amesikika katika kipindi cha XXL kinachorushwa na kituo cha habari cha Clouds Fm, Jay Mo alisema kwamba wasanii wengi wanaenda kufanya video nje kwa mkumbo kwa kuona Fulani amefanya, pasipo kua na malengo yakinifu.
Aliendelea na kusema kuwa ni vyema wasanii wajue wanapoenda kufanya kazi nje wajue wanalenga soko la wapi, na sio kukurupuka. Hivyo msanii anaweza akafanya video ndani ya nchi na kuteka soko la ndani halikadhalika na la nje pia.
Weekly Top 10 songs

omelette4:28
ONLY YOU JESUS5:44
Melody Ft Tunche the best3:20
Kupenda nishapenda zaani3:12
Nigina2:27
R.I.P Manu4:52
CHAMPION GAL3:00
Zabike2:50
Haipo Sawa (Feat. Don breezy)4:13
Wano Wano2:15
Top stories
- OXEN MUSIC
29 July
- Mytee boy - SURVIVE
28 July
- Abakuchinsali
29 July


Leave your comment