Exclusive DJ Mixes and 100% Ad-Free Music!
TANZANIA: Dayna Nyange asema hajawahi kufikiria kudate na wasanii..
15 February 2016

Msanii wa muziki, Dayna Nyange amesema hawezi kutoka kimapenzi na wasanii wa bongo kutokana na kuwa na wivu.
Mrembo huyo ambaye pia ni mzazi wa mtoto mmoja aitwaye ‘Rahma’, amekiambia kipindi cha XXL cha Clouds FM kuwa hapendi kuwa na mahusiano na mastaa kwasababu wengi wana mambo mengi.
“Sijawahi kufikiria ‘kudate’ na wasanii kwasababu nawaogopa, ni pasua kichwa. Mimi nina wivu sana mazingira tuliyonayo nadhani nitakonda mara mia”, alisema Dayna Nyange.
Dayna Nyange ni kati ya wasanii wakike ambao hwapendi kuweka mambo ya mahusiano yao public.
Weekly Top 10 songs
Top stories
- SHUKRANI
02 May
- DJ GALIK PRO
02 May




Leave your comment