TANZANIA: Watayarishaji muziki hatuna umoja - Master Jay

<p style="text-align: justify;"><img src="/media/articles/1453986792_1281_b.jpg" alt="" /></p>
<p style="text-align: justify;">&nbsp;</p>
<p style="text-align: justify;">Mtayarishaji mkongwe wa muziki nchini, Master J amesema siku umoja wa watayarishaji muziki nchini ukiundwa, atarudi rasmi kutayarisha muziki.</p>
<p style="text-align: justify;">Master J ambaye ni mmiliki wa MJ Records, aliliambia gazeti la Mwananchi kuwa, mfumo uliopo kwenye tasnia ndiyo unaochangia kwa kiasi kikubwa kuondoa thamani ya watayarishaji.</p>
<p style="text-align: justify;">&ldquo;Watayarishaji muziki na waongozaji video wana umuhimu mkubwa katika kukuza muziki hapa nchini, lakini niseme wazi kwamba hatuna maana kutokana na kukosekana kwa umoja baina yetu&rdquo;, alisema.</p>
<p style="text-align: justify;">&ldquo;Niliwahi kuitisha kikao kwa lengo la kuunda umoja, ikashindikana. Nimeamua kukaa kando kwa muda ili mambo yakinyooka nirudi upya&rdquo;</p>
<p style="text-align: justify;">Master J alidai kuwa kutokana na kukosa umoja, kunawafanya watayarishaji wengi wa muziki waonekane hawana maana halia inayowafanya kugawa midundo yao bure.</p>

Leave your comment

Top stories