EXCLUSIVE (TANZANIA) – Nilianza kuitwa baba tangu nikiwa kidato cha pili – Nay Wa Mitego

<p style="text-align: justify;"><img src="/media/articles/1453290591_2773_b.jpg" alt="" /></p>
<p style="text-align: justify;">&nbsp;</p>
<p style="text-align: justify;">Msanii wa Bongo Fleva, Nay Wa Mitego alianza kuitwa baba akiwa kidato cha pili.</p>
<p style="text-align: justify;">Mambo hayo yalitokea baada ya kumzalisha msichana wa kihindi aliyefukuzwa kwao na kuwalazimu kutafuta chumba cha kupanga na kuishi pamoja wakati Nay akiendelea kusoma sekondari.</p>
<p style="text-align: justify;">Ambapo hiyo pia ilitokea miaka michache baada ya kuwa amefukuzwa kwao akiwa darasa la saba na kwenda kuishi salon.</p>
<p style="text-align: justify;">&ldquo;Nilipofika form two nilikutana na mwanamke wa kihindi ambaye ndiye nimezaa naye mtoto wa kwanza aliyekuwa ananisaidia ada&rdquo;, amesema Nay kwenye kipindi cha Chill na Sky.</p>
<p style="text-align: justify;">Nay anasema baada ya girlfriend wake kufukuzwa kwao walienda kutafuta nyumba ya kupanga Manzese lakini walishindwa kupata chumba kwakuwa walionekana wadogo sana kiumri.</p>
<p style="text-align: justify;">Anasema walibidi waende kutafuta chumba maeneo ya Kimara ambako walifanikiwa. Nay anasema girlfriend wake alimsaidia fedha ya ada pamoja na hela ya kwanza kwenda kurekodi wimbo wake kwa P-Funk.</p>
<p style="text-align: justify;">Sikiliza kipindi kizima cha Chill na Sky hapa chini;</p>
<p style="text-align: justify;"><iframe src="http://www.audiomack.com/embed4-large/bongofive/nay-wa-mitego" width="100%" height="265" frameborder="0" scrolling="no"></iframe></p>

Leave your comment

Top stories