Exclusive DJ Mixes and 100% Ad-Free Music!
EXCLUSIVE (TANZANIA) – Mandojo na Domokaya waja na Studio mpya
11 January 2016

Wasanii wa muziki, Mandojo na Domokaya wamefungua studio mpya mbali na uwekezaji wanaoufanya katika biashara zao mbalimbali. Wameamua kufungua studio kwa lengo la kuwasaidia wasanii wengine kufikia mafanikio kimuziki.
Akizungumza katika kipindi cha E News cha East Africa Television, Mandojo alisema studio yao tayari imeshaanza kufanya kazi.
“Sisi kwa sasa hivi studio tumeshaifungua ipo kinondoni. Domokaya ndiyo yupo pale anasimamia kwasababu tunakuwa na producer tofauti tofauti yaani hata kama msanii ana producer wake anaweza akaja nae”, alisema Mandojo.
“Pia tayari kuna wasanii ambao tupo nao ndani ya label na tukiona kuna wasanii wengine wana uwezo tunawasaini. Sasa hivi tunataka kufanya muziki wa kitofauti kidogo kwasababu mwanzoni tulishafanya harakati za muziki. Kwahiyo sasa tunataka tuwekeze nguvu zetu kwenye huu muziki wa bongo fleva hasahasa kusaidia vijana wapya ambao hawajapata nafasi”, aliongeza Mandojo.
Mandojo na Domokaya waliwahi kutamba na nyimbo kama Nikupe nini, Wanoknok na nyingine.
Weekly Top 10 songs

Black Mark utandilubi omwami wangu5:21
KAPEKE LONDON2:23
In My Bed2:50
Paver2:55
CHAMPION GAL3:00
Ex Nkubilako ft DonMusa2:55
BIkola2:58
The Prelude of Grace1:31
Joy Is Coming3:08
Worship My King5:00
Top stories
- Excellent Jesus
26 May
- Angel Prince Biography
27 May
- Grateful
25 May


Leave your comment