Exclusive DJ Mixes and 100% Ad-Free Music!
EXCLUSIVE (TANZANIA) – Kushoot video nje ya nchi ni usaliti – Afande Sele
23 December 2015

Msanii mkongwe nchini Afande Sele amedai kuwa anawashangaa wasanii wanaoenda kushoot video zao nje ya nchi, wakati Tanzania ina kila kitu.
Rapa huyo mkongwe aliyekuwa kimya kwa muda kutokana na shughuli za kampeni, amesema kuwa anaamini wasanii wanaosafiri kwaajili ya kushoot video nje ya nchi, wana biashara zao za siri na ni usaliti.
“Kwenda kushoot video nje ya nchi ni ulimbukeni” alisema Afande Sele.
“Tanzania tuna kila kitu kuliko hata huko wanakoenda, Mimi hii naitafsiri kama usaliti wa nchi, sisi tunakosa nini hapa nyumbani? Tuna milima, mbuga, maporomoko mazuri, yaani tuna kila kitu. Unajua wasanii wengi walikuwa wanatumia mwanya wa kwenda kushoot video nje ili kufanya biashara zao za siri. Wengi wametumia sana huu mwanya, sasa Magufuli alivyoingia atawanyoosha tu”, aliongea Rapa huyo.
Pia Afande Sele ameongeza kuwa anajipanga kuachia nyimbo mpya mbili kufidia ukimya mkubwa aliouacha kwa mashabiki wake.
Source: Bongo 5
Weekly Top 10 songs

Black Mark utandilubi omwami wangu5:21
KAPEKE LONDON2:23
In My Bed2:50
Paver2:55
CHAMPION GAL3:00
Ex Nkubilako ft DonMusa2:55
BIkola2:58
The Prelude of Grace1:31
Joy Is Coming3:08
Worship My King5:00
Top stories
- Excellent Jesus
26 May
- Angel Prince Biography
27 May
- Grateful
25 May


Leave your comment