Exclusive DJ Mixes and 100% Ad-Free Music!
EXCLUSIVE (TANZANIA) – C9 kuingia mkataba na Panamusiq
20 November 2015

Kampuni ya kusimamia wasanii wa muziki Panamusiq wanayofuraha kuwajulisha kuwa Producer mkubwa Tanzania Charles Francis ( C9 ), ameingia mkataba wa muda mrefu pamoja na kampuni hiyo kwa Dar es salaam.
Charles Francis ni mtoto wa mwisho katika familia ya kitanzania yenye watoto 9 (jina la kisanii C9) na mtayarishaji anayeheshimika kwa kazi zake nzuri, kama Mbona Silali (Rich Mavoko), Amerudi (Christian Bella/ Malaika Band), Suna (Barnaba), Mtima Wange (Amini ft Linah) na Dudu (Shilole ft Q. Chillah).
Alianza kuendeleza fani yake ya uprodyuza kwa kufanya kazi na Chuchu FM ya Zanzibar ambapo alikuwa akitengeneza matangazo. Na baadaye alifanya kazi na KIRI records na kisha kuamua kuanzisha studio yake mwenyewe inayoitwa C9 Rekodz.
Kipaji cha C9 kilitambulika pale alipochaguliwa kuwania tuzo za Tanzania Kilimanjaro Music Awards katika kipengele cha ProducerBora wa Mwaka 2013/2014.
Katika mkataba huo Panamusiq wamesema kuwa kutakuwa na muunganiko mkubwa katika kutengeneza na kutoa miziki ya kiafrika yenye viwango bora. Wasanii wengine ambao wapo chini ya Panamusiq ni Linah, Feza na Kioo ambaye ni msanii mpya atayetoa nyimbo zake mapema mwakani 2016.
Taarifa zaidi katika kusign na wasanii zitatoka hivi karibuni.
Source: Panamusiq press release.
Weekly Top 10 songs

Black Mark utandilubi omwami wangu5:21
KAPEKE LONDON2:23
In My Bed2:50
Paver2:55
CHAMPION GAL3:00
Ex Nkubilako ft DonMusa2:55
BIkola2:58
The Prelude of Grace1:31
Joy Is Coming3:08
Worship My King5:00
Top stories
- Excellent Jesus
26 May
- Angel Prince Biography
27 May
- Grateful
25 May


Leave your comment