Exclusive DJ Mixes and 100% Ad-Free Music!
Jaivah Akutana Na Chley Nkosi Wa Afrika Kusini, Adokeza Ngoma Mpya
19 March 2024

Image Source: Online
Writer: Charles Maganga
Baada ya ukimya wa takriban miezi minne hatimaye nyota kutokea lebo ya Bxtra Records, Jaivah amedokeza ujio wake mpya hivi karibuni.
Mara ya mwisho kwa Jaivah kuachia ngoma ilikuwa ni mwezi Desemba mwaka 2023 ambapo aliachia Buruda ambayo alimshirikisha Marioo, ngoma ambayo kufikia sasa imeshatazamwa takriban mara Milioni 3 kwenye mtandao wa YouTube.
Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Jaivah alipost picha inayomuonesha akiwa na msanii kutokea Afrika Kusini, Chley Nkosi na kisha kudokeza kuwa ataachia ngoma mpya ya kuitwa Kautaka hivi karibuni.
Chley Nkosi si jina jipya katika muziki wa Tanzania kwani msanii huyo kutoka Afrika Kusini tayari alishafanya collabo na wasanii wawili wakubwa kutoka Tanzania, Diamond Platnumz kwenye "Shu!" na Mbosso kwenye "Sele".
Weekly Top 10 songs
Top stories
- Diso Ziod
21 April
- Lesson
20 April
- Drop new song loyo
21 April




Leave your comment