Exclusive DJ Mixes and 100% Ad-Free Music!
Diamond Platnumz Athibitisha Kushiriki Kwenye Albamu Mpya Ya Sholo Mwamba
28 February 2024

Image Source: Online
Writer: Charles Maganga
Mshindi mara tatu wa tuzo za MTV EMA, Diamond Platnumz hivi karibuni amethibitisha kuwa atashiriki kwenye albamu ya Sholo Mwamba ambayo iko mbioni kuingia sokoni.
Sholo Mwamba hivi karibuni anatarajiwa kuachia albamu yake ya muziki na hivi karibuni Diamond Platnumz amethibitisha kuwa atakuwepo kwenye albamu ya msanii huyo mwenye miondoko ya Singeli.
Katika kuonesha kuungana mkono albamu hiyo, Diamond Platnumz kupitia Insta story yake alidokeza kuwa ni lazima ashiriki kwenye albamu hiyo.
“Mwamba The Rock. My Home Boy Brother, Love Always. Inshaallah Lazima Niwepo Kwenye Albamu Hiyo Mwanangu” aliandika Diamond Platnumz
Ahadi hii ya Diamond Platnumz inabidi kudhihirisha kuwa kwa sasa Diamond Platnumz ataendelea kufanya collabo na wasanii wa nyumbani baada ya hivi karibuni kufanya ngoma na Mr Blue, Jay Melody, Jux na wengineo wengi.
Weekly Top 10 songs
Top stories
- Playlist my upcoming song
30 March
- ITSLILREMY
30 March
- Usman Khalifa Amoto
30 March
- Ingopangani Download nyimbozi
30 March




Leave your comment