Exclusive DJ Mixes and 100% Ad-Free Music!
Mario Adokeza Collabo Nyingine Na Ali Kiba
25 May 2023

Picha: Instagram
Mwandishi: Charles Maganga
Fundi wa muziki kutoka Tanzania Marioo hivi karibuni ameingia kwenye vichwa vya habari nchini baada ya kudokeza ujio wa collabo mpya kati yake na CEO wa Kings Music Ali Kiba.
Siku ya Jumapili wawili hao yaani Ali Kiba na Marioo walitumbuiza pamoja kwenye tamasha la “Reloaded” ambalo pia lilisindikizwa na msanii nguli kutoka Nigeria wa kuitwa Ayra Starr.
Mara baada ya tamasha hilo kumalizika, Marioo alitumia ukurasa wake wa Instagram kudokeza ujio wa ngoma yake mpya na Ali Kiba ambapo aliandika kwa kumsihi Ali Kiba atoe wimbo huo waliofanya pamoja kwani amechoka kukaa na “Hit” ndani.
“Mfalme Ali Kiba” Dondosha lile banger. Naona kama Nashindwa kuvumilia kukaa na hit ndani” aliandika Marioo kwenye ukurasa wake wa Instagram. Katika ujumbe wake huo Marioo hakutaja jina la ngoma wala tarehe ambayo ngoma hiyo inatarajiwa kuachiwa.
Ikumbukwe kuwa Marioo na Ali Kiba wameshafanya collabo ya pamoja kwenye “I Miss” ngoma ambayo inapatikana kwenye albamu ya Marioo ya kuitwa “The Kid You Know” ambayo iliachiwa mwishoni mwa mwaka 2022.
Weekly Top 10 songs

Kamwambie3:47
chile-one-so-lucky4:02
Joy Is Coming3:08
TUMWAMBIE MUNGU ASANTE0:49
Malaika2:49
NALOKINGA2:52
Stima - Buruklyn Boyz5:04
Baddie remix feat Shannnon, aaronix, Tojo3:14
Buwooma2:44
Alifata Hela3:53
Top stories
- NEW MANAGEMENT
01 April
- Love
01 April
- My biography
02 April
- STREAM NEXARITO SONGS ON SPOTIFY
02 April


Leave your comment