Exclusive DJ Mixes and 100% Ad-Free Music!
Nyimbo Mpya Tanzania na Kenya Wiki Hii
22 May 2023

Picha Kutoka Instagram
Mwandishi: Charles Maganga
Ndani ya wiki hii, wasanii tofauti tofauti kwenye kiwanda cha muziki Tanzania wameendelea kupba kiwanda cha Bongo Fleva kwa nyimbo kali zenye mahadhi tofauti tofauti kama Hip Hop, Bongo Fleva na aina nyingine za muziki.
Kutoka kwa wasanii kama Nandy, Nay Mitego na wengineo wengi, hizi hapa ni ngoma mpya Tanzania wiki hii :
On Fire - Ali Kiba
Baada ya kuburudisha mashabiki na “Mahaba” mapema mwaka huu, Ali Kiba amerudi tena na “On Fire” ngoma ambayo Kiba anaeleza kwa undani namna ambavyo penzi limemnogea na namna ambavyo ana furaha kwa sasa.
Falling - Nandy
Kwenye ngoma mpya ya Nandy utapata mashahiri mujarab ya mapenzi lakini pia utarahani mdundo mkali kutoka kwa Kimambo beats ambaye ndiye ametayarisha “Falling” ambayo ni ngoma ya kwanza kutoka kwa Nandy kwa mwaka 2023.
Yanga Anthem 2 - Marioo
Marioo kwa mara nyingine aliamua kukosha mashabiki wa Yanga na wimbo wake wa “Yanga Anthem 2” ambao ndani yake fundi huyo Bongo Fleva amesifia haswa klabu ya Yanga ambayo ni moja kati ya klabu za soka nchini Tanzania.
Tushaachana - Chiby & Mabantu
Kwenye wimbo huu Mabantu kwa maneno mepesi sana wameeleza dhana ya “Friends For Benefit” ambapo humu ndani wakali hawa wanaweka wazi kuwa wameshaachana na wapenzi wao wa zamani lakini bado wanaendeleza kwa siri mahusiano yao.
Funga Kazi - Manengo Ft Darassa
Muziki wa Hiphop ulipata zawadi wiki hii kutoka kwa Manengo akiwa na Darassa kupitia “Funga Kazi” wimbo mkali wa rap ambao ndani yake Manengo na Darassa wanazungumzia mambo mbalimbali ya kila siku.
"
Weekly Top 10 songs

Kamwambie3:47
chile-one-so-lucky4:02
Joy Is Coming3:08
TUMWAMBIE MUNGU ASANTE0:49
Malaika2:49
NALOKINGA2:52
Stima - Buruklyn Boyz5:04
Baddie remix feat Shannnon, aaronix, Tojo3:14
Buwooma2:44
Alifata Hela3:53
Top stories
- NEW MANAGEMENT
01 April
- Love
01 April
- My biography
02 April
- STREAM NEXARITO SONGS ON SPOTIFY
02 April


Leave your comment