Exclusive DJ Mixes and 100% Ad-Free Music!
Ngoma Mpya Tanzania: Jux Afichua DJ Ally B Kushiriki Kwenye Ngoma Yake
17 May 2023

[Picha: Instagram]
Mwandishi-Charles Maganga
DOWNLOAD LATEST BONGO MUSIC MP3
Kama kuna ngoma ambayo kwa sasa inasumbua kwenye klabu na mitandao ya kijamii basi bila shaka ni ngoma ya kwake Jux ya kuitwa “Shuga Daddy” ambayo amefanya na DJ Tarico pamoja G Nako.
Sasa hivi karibuni Juma Jux amefichua kuwa DJ maarufu kwa sasa nchini Tanzania, DJ Ally B pia amehusika katika kuandaa ngoma hiyo yenye miondoko ya Amapiano.
DJ Ally B ni moja kati ya Ma-DJ bora na maarufu kutoka Tanzania kwa sasa ambapo hivi karibuni alishinda tuzo ya DJ Bora Wa Kiume Wa Mwaka kwenye Tuzo Za Tanzania Music Awards 2023.
Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Jux aliweka video inayomuonesha DJ Ally B akiwa anaweka anarekodi studio ambapo DJ huyo anayetokea mkoani Moshi alionekana akiwa anapuga miluzi na kuweka vionjo vyake kwenye wimbo huo.
“Thank you so much my brother DJ Ally B Kama ulikuwa haujui kwenye Shuga Daddy nakujuza. MIRUZII imepigwa na BINGWA wa miruzi Nchini Dokta DJ Ally B” aliandika msanii huyo.
Weekly Top 10 songs

In My Bed2:50
KAPEKE LONDON2:23
BIkola2:58
Buwooma2:44
Baddie remix feat Shannnon, aaronix, Tojo3:14
Paver2:55
Nitampeleka kwa Mama (ft. Xouh)3:44
Ex Nkubilako ft DonMusa2:55
CHAMPION GAL3:00
Kamwambie3:47
Top stories
- UPCOMING EP FROM EMKAY64
14 May
- Daniel Sifuna
14 May
- Generation
16 May
- NEW SONG ALERT
16 May


Leave your comment