Exclusive DJ Mixes and 100% Ad-Free Music!
Hatimaye Rayvanny Aachia FLOWERS III Tanzania
15 May 2023

[Picha: Instagram]
Mwandishi-Charles Maganga
DOWNLOAD LATEST BONGO MUSIC MP3
Mwanamuziki kutoka Tanzania, Rayvanny hatimaye ameachia EP yake iliyokuwa ikisubiriwa kwa hamu sana na mashabiki ya kuitwa Flowers III
Flowers III ni EP ya tatu katika mtiririko wa Flowers EP kutoka kwa mshindi huyo wa tuzo za BET. Flowers ya kwanza ilitoka mwaka 2020 huku Flowers II ikiwa imeachiwa mwaka 2022 ambapo Rayvanny aliwashirikisha wasanii kama Zuchu, Ray C na Marioo.
Kwenye Flowers III Rayvanny ametengeneza ngoma 9 ambapo 3 kati ya hizo ambazo ni “Forever” “One Day Yes” na “Mwambieni” tayari zimeshatoka. Aidha kwenye EP hii Rayvanny ameshirikisha wasanii tofauti tofauti tofauti ikiwemo Phina, Jay Melody, Mac Voice na Bahati kutoka Kenya.
Ikumbukwe kuwa kufikia sasa Rayvanny ana jumla ya EP 5 pamoja na albamu moja ambayo ni Sounds From Africa ya mwaka 2021.
Weekly Top 10 songs

Tudo Trocado3:17
CHAMPION GAL3:00
ONLY YOU JESUS5:44
Akaana kokukyalo2:21
Joy Is Coming3:08
Nasema3:02
BESTIE2:26
Minha Historia3:41
Baraka4:33
Nigina2:27
Top stories
- MCHUNGAJI
07 July
- News Flash
09 July


Leave your comment