Exclusive DJ Mixes and 100% Ad-Free Music!
Baba Levo Athibitisha Kumshirikisha Diamond Platnumz Kwenye Ep Yake
5 April 2023

[Picha: Instagram]
Mwandishi: Charles Maganga
Pata Habari za Muziki na Mixtapes Kwenye Telegram
Msanii kutoka Tanzania na mtangazaji wa Wasafi FM Baba Levo hivi karibuni amethibitisha kwamba amemshirikisha Diamond Platnumz kwenye EP yake.
Baba Levo ambaye alishawahi kuwa Diwani kabla ya kuingia kwenye utangazaji amethibitisha kuwa Simba ni moja ya wasanii ambao wapo kwenye EP yake anayotarajia kuiachia hivi karibuni. Baba Levo amekuwa akidokeza kwa muda mrefu sasa kuhusu ujio wa EP hiyo ambayo inaitwa 'Seven Wonders EP.'
Kwenye video ambayo inasambaa kwa kasi sana kwa sasa kwenye mitandao ya kijamii, Baba Levo alionekana akimsihi Diamond Platnumz kwamba asikilize ngoma yake mpya ambayo wamefanya pamoja kupitia zawadi ya Spika aliyompatia.
“Diamond Sikiliza ngoma yangu mpya aliyonisaidia aisikilizie humu” alisikika akisema Baba Levo kwenye video hiyo.
Ikumbukwe kuwa Diamond Platnumz na Baba Levo tayari wana ngoma ambayo inaitwa Shusha ambayo ilitoka mwaka 2021.
Weekly Top 10 songs

Trust No One3:13
chile-one-so-lucky4:02
Kamwambie3:47
Joy Is Coming3:08
Buwooma2:44
Udede Ft Msomali x Malume & Samas Alifata Hela Remix6:34
Msaliti 11:25
Leo3:39
Maringo4:00
NANI ft. Kamanda Pedeshee3:56
Top stories
- The Marathon
25 April
- Who Is Bad Beric
24 April
- Cashout by monyzoh boy
24 April
- MOSS Kay
24 April


Leave your comment