Exclusive DJ Mixes and 100% Ad-Free Music!
Baba Levo Athibitisha Kumshirikisha Diamond Platnumz Kwenye Ep Yake
5 April 2023

[Picha: Instagram]
Mwandishi: Charles Maganga
Pata Habari za Muziki na Mixtapes Kwenye Telegram
Msanii kutoka Tanzania na mtangazaji wa Wasafi FM Baba Levo hivi karibuni amethibitisha kwamba amemshirikisha Diamond Platnumz kwenye EP yake.
Baba Levo ambaye alishawahi kuwa Diwani kabla ya kuingia kwenye utangazaji amethibitisha kuwa Simba ni moja ya wasanii ambao wapo kwenye EP yake anayotarajia kuiachia hivi karibuni. Baba Levo amekuwa akidokeza kwa muda mrefu sasa kuhusu ujio wa EP hiyo ambayo inaitwa 'Seven Wonders EP.'
Kwenye video ambayo inasambaa kwa kasi sana kwa sasa kwenye mitandao ya kijamii, Baba Levo alionekana akimsihi Diamond Platnumz kwamba asikilize ngoma yake mpya ambayo wamefanya pamoja kupitia zawadi ya Spika aliyompatia.
“Diamond Sikiliza ngoma yangu mpya aliyonisaidia aisikilizie humu” alisikika akisema Baba Levo kwenye video hiyo.
Ikumbukwe kuwa Diamond Platnumz na Baba Levo tayari wana ngoma ambayo inaitwa Shusha ambayo ilitoka mwaka 2021.
Weekly Top 10 songs

In My Bed2:50
KAPEKE LONDON2:23
BIkola2:58
Buwooma2:44
Baddie remix feat Shannnon, aaronix, Tojo3:14
Paver2:55
Nitampeleka kwa Mama (ft. Xouh)3:44
Ex Nkubilako ft DonMusa2:55
CHAMPION GAL3:00
Kamwambie3:47
Top stories
- UPCOMING EP FROM EMKAY64
14 May
- Daniel Sifuna
14 May
- Generation
16 May
- NEW SONG ALERT
16 May


Leave your comment