Exclusive DJ Mixes and 100% Ad-Free Music!
Diamond Platnumz Na Billnass Waandika Historia Mwezi Machi
4 April 2023

[Picha: Instagram]
Mwandishi: Charles Maganga
Pata Habari za Muziki na Mixtapes Kwenye Telegram
Wasanii kutoka nchini Tanzania Diamond Platnumz na rapa Billnass wameandika historia mwezi Machi baada ya kufanya vizuri kwenye mtandao Youtube kwa mwezi huo.
Diamond Platnumz ambaye kwa mwaka wa 2023 ameshaachia ngoma 2 kwa mara nyingine ameweka rekodi mpya Youtube kwa mwezi Machi huku Billnass akiwa ameongoza kwenye orodha ya wasanii wa Hiphop Tanzania waliofanya vizuri kwenye mtandao huo.
Kwa mwezi Machi pekee Diamond Platnumz amekusanya views Milioni 31 kwenye mtandao na hivyo kuwa msanii wa Tanzania aliyetazamwa zaidi kwa mwezi huo. Kwenye orodha hiyo iliyotolewa na Charts Tanzania Harmonize anashika nafasi ya pili akiwa na views Milioni 14, Rayvanny, Zuchu na Ali Kiba pia waling’ara kwenye orodha hiyo.
Kwa uplande wa Hip Hop Billnass alikusanya views Milioni 2.52 hivyo kuwa Msanii wa Hip Hop aliyetazamwa zaidi YouTube kwa mwezi Machi. Darassa, Stamina Shorwebwenzi, Nay Wa Mitego na Kontawa ni Baathist ya wasanii waliotajwa pia kwenye orodha hiyo.
Weekly Top 10 songs

Trust No One3:13
chile-one-so-lucky4:02
Kamwambie3:47
Joy Is Coming3:08
Buwooma2:44
Udede Ft Msomali x Malume & Samas Alifata Hela Remix6:34
Msaliti 11:25
Leo3:39
Maringo4:00
NANI ft. Kamanda Pedeshee3:56
Top stories
- The Marathon
25 April
- Who Is Bad Beric
24 April
- Cashout by monyzoh boy
24 April
- MOSS Kay
24 April


Leave your comment