Nyimbo Zinazotamba Tanzania Wiki Hii

[Picha: Instagram]

Mwandishi: Charles Maganga

Pata Habari za Muziki na Mixtapes Kwenye Telegram

Bongo Fleva inazidi kuchangamka kutokana na ushindani ambao upo baina ya wasanii hasa katika suala zima la kutoa ngoma kali na katika wiki hii ya mwisho ya mwezi Machi zifahamu ngoma ambazo zimeteka na kufanya zaidi hapa nchini Tanzania kwenye mtandao wa Youtube

Kutoka kwa Harmonize mpaka kwa Darassa zifahamu ngoma kali zinazofanya vizuri hapa Tanzania kwenye mtandao wa Youtube

Single Again - Harmonize

Ufundi wa Director Kenny umeonekana barabara kwenye video hii ya Harmonize ya kuitwa “Single Again” ambayo kufikia sasa imeshakusanya watazamaji takriban Milioni 1.2 Youtube tangu kuachiwa kwake

https://www.youtube.com/watch?v=5YbLZjoiRho

 

Jua Lile - Nacha Ft Stamina

Ngoma hii “Jua Lile” inaweza kusikilizwa na yeyote kwani ndani ya mkwaju huu Nacha na Stamina wamepiga stori nyingi sana kuhusu maisha ya kila siku, muziki wa Tanzania na mambo mengine nengi sana.

https://www.youtube.com/watch?v=UICNQEJnHC0

 

Napambana - Zuchu

Ngoma hii ya Zuchu imeendelea kupambania kombe ili kuweza kuendelea kushika nafasi za juu kwenye Youtube. Tangu kuachiwa kwake “Napambana” ya Zuchu imeshakusanya watazamaji Milioni 2.7 Youtube

https://www.youtube.com/watch?v=WpvN2fDsqsg

Nani? - Abigail Chams Ft Marioo

Kwenye Amapiano hii mujarab, Abigail Chams na Marioo wanasifiana, wanapongezana na kutupiana maneno matamu ili tu kunogesha mahusiano yao. Wengi wamependa ngoma hii kutokana na beat kali na muingiliano mzuri wa sauti baina ya wawili hawa

https://www.youtube.com/watch?v=qNY1CxGKiEI

Mind Your Business - Darassa

Ngoma ya Darassa “Mind Your Business” inazidi kupepea. Kwenye ngoma hii utapenda mashahiri mazuri kutoka kwa Darassa pamoja na video fupi na isiyoboa ambayo ndani yake anaonekana DJ maarufu kutoka Tanzania, DJ Ally B

https://www.youtube.com/watch?v=8qVDDDoT0rY

Leave your comment