Video Za Harmonize Zilizotazamwa Zaidi

[Picha: Instagram]

Mwandishi: Charles Maganga

Pata Habari za Muziki na Mixtapes Kwenye Telegram

Nchini Tanzania, Harmonize ndiye msanii wa tatu, nyuma ya Diamond Platnumz na Rayvanny kwa kuwa na wafuasi (subscribers) wengi zaidi Youtube huku Chanel yake ikiwa imeshatazamwa takriban mara Milioni 878 kwenye mtandao huo.

Kupitia makala hii tunaenda kuzihesabu video 5 za muziki kutoka kwa Harmonize zilizotazamwa zaidi kwenye chaneli yake ya Youtube

Kwangaru Featuring Diamond Platnumz

Kwangaru ndio ngoma ya Harmonize iliyotazamwa zaidi Youtube ambapo kufikia sasa imeshakusanya watazamaji Milioni 102 kwenye mtandao wa Youtube. Video ya Kwangaru ilitoka mwaka 2018 na ilitayarishwa na Director Kenny

https://www.youtube.com/watch?v=0Wbc5ZwkAMw

Happy Birthday

Happy Birthday ni moja kati ya ngoma maarufu sana kutoka kwa Harmonize na kufikia sasa imeshatazamwa mara Milioni 41 kwenye mtandao wa Youtube.

https://www.youtube.com/watch?v=l9O_SFcH4Kk

Bado Featuring Diamond Platnumz

Bado ilikuwa ni video ya pili kutoka kwa Harmonize tangu kusainiwa WCB Wasafi na kutokana na stori ya video hii kuwa kali wengi walivutiwa na video hii ambayo kufikia sasa imeshatazamwa mara Milioni 36. Video ya Bado ilifanyika Afrika Kusini na iliongozwa na Nicklass.

https://www.youtube.com/watch?v=M6PJp1p6BLg

Aiyola

Aiyola ndio ngoma na video iliyomtambulisha Harmonize kwenye uwanja wa Bongo Fleva na kufikia sasa video hii imeshatazamwa mara Milioni 28 kwenye mtandao wa Youtube

https://www.youtube.com/watch?v=sWPqjpXgl08

Magufuli 

Kwenye ngoma hii, Harmonize alilenga kumpa sifa kedekede aliyekuwa Rais Wa Tanzania, John Pombe Magufuli na ili kufanya hivyo, Harmonize aliufanyia remix wimbo wa “Kwangaru” ambapo aliisindikiza ngoma hiyo na video kali ambayo kufikia sasa imeshakusanya views Milioni 28 Youtube.

https://www.youtube.com/watch?v=FrAZ5Lzf5AU

Leave your comment