Exclusive DJ Mixes and 100% Ad-Free Music!
Stamina Aachia Ngoma Mpya Machozi Ft Bushoke
24 February 2023

[Picha: Instagram]
Mwandishi: Charles Maganga
Pata Habari za Muziki na Mixtapes Kwenye Telegram
Rapa mwenye heshima yake kwenye muziki wa Tanzania Stamina Shorwebwenzi amerudi kivingine na ngoma yake mpya ya kuitwa Machozi akiwa amemshirikisha Bushoke.
Kama kuna kitu ambacho mashabiki wanafahamu kuhusu Stamina basi ni uwezo wake wa kuandika ngoma zenye ujumbe zilizonakshiwa na hadithi nzuri na baadhi ya ngoma hizo ni pamoja na Ukizaliwa, Future Wife na Baba.
Kwenye Machozi Stamina analalamika kuhusu mkewe ambaye sio mwaminifu kwenye mahusiano. Humu ndani utasikia kwa upana na marefu malalamiko yake kuhusu namna ambavyo mkewe anachepuka nje ya ndoa na namna ambavyo Stamina kama mume, alikuwa anajitahidi kutunza familia yake.
Hii ni ngoma ya kwanza kwa Stamina kwa mwaka huu na imetayarishwa na Sampamba kutoka Tanzania.
Weekly Top 10 songs
Top stories
- The Marathon
25 April
- Cashout by monyzoh boy
24 April
- TRUE LOVE
26 April
- O Daynor pisom 03 casou
24 April




Leave your comment