‘Yanga Tamu’ Marioo, ‘Take One’ Country Wizzy na Nyimbo Zingine Mpya Tanzania Wiki Hii

[Picha: EATV]

Mwandishi: Charles Maganga

Pata Habari za Muziki na Mixtapes Bure Kwenye Telegram

Kila wiki wasanii kutoka Tanzania wamekuwa wakichangamsha kiwanda cha Bongo Fleva kwa kutoa ngoma mpya kabisa ambazo zimekuwa zikiuhisha wafuasi wao.Zifuatazo ni ngoma tano kali mpya ambazo zimetikisa kiwanda cha Bongo Fleva kwa wiki hii:

Pakua nyimbo za Marioo Bila Malipo Kwenye Mdundo

Nobody - Walter Chilambo

Kwenye ‘Nobody’, Walter Chilambo anatumia kipawa cha sauti yake kusimulia ukuu wa Mungu kwenye maisha yake na namna ambavyo huruma na upendo wa mwenyezi Mungu umemzunguka.

https://www.youtube.com/watch?v=0CijcQyzf3g

Yanga Tamu - Marioo

Kama uliipenda ‘Bia Tamu’ kutoka kwa Marioo, basi bila shaka pia utaipenda ‘Yanga Tamu’ ambayo ni kama remix ya Amapiano hiyo. Kwenye ‘Yanga Tamu’, Marioo anaisifia sana klabu ya Yanga ambayo ni mojawapo ya klabu kubwa za soka hapa nchini Tanzania.

https://www.youtube.com/watch?v=ERkUsjhXS_k

Tanzanite - Joh Makini

Kitu kinachovutia zaidi kwenye ‘Tanzanite’ ni namna ambavyo Joh Makini ameweza kurap kwa kiswahili lakini pia akiweka vionjo vya maneno ya kiingereza kitu ambacho kinafanya ngoma hii ambayo imetayarishwa na Switch kuweza kuwa na mzuka wa kitofauti sana.

https://www.youtube.com/watch?v=HFgapoqIHvw

Take One - Country Wizzy

Country Wizzy amezidi kuimarisha ufalme wake kwenye muziki wa trap kwa kuachia mkwaju wake wa ‘Take One’ ambao bila kujali umri, jinsia na ushabiki ni sahihi kusema kuwa mashahiri ya ngoma hii yanaweza kumfanya yeyote aimbe na kuruka pindi atakapoisikiliza.

https://www.youtube.com/watch?v=LSPkFxHmy90

The Green Light (EP) - Killy

Ukiweka kando collabo kutoka kwa wasanii kama Ibraah, Christian Bella na Harmonize kitu kingine ambacho kinafanya EP ya Killy ya kuitwa ‘The Green Light’ kuwa bora ni mpngilio mzuri wa ngoma, ubora wa sauti uliotumika ambao ni wa hali ya juu pamoja na mashairi. Hii ni EP ya kwanza kutoka kwa Killy tangu aanze muziki na pia ni EP ya tatu kuachiwa ndani ya lebo ya Konde Gang baada ya ‘Steps’ na ‘Karata Tatu’ za Ibraah kufanya vizuri. 

https://www.youtube.com/watch?v=yH1vUatImkA

Leave your comment