Exclusive DJ Mixes and 100% Ad-Free Music!
Nyimbo Mpya Zilizoachiwa na Ibraah, Nandy na Maua Sama Tanzania Wiki Hii
29 November 2021

[Picha: The Standard]
Mwandishi: Charles Maganga
Pata Habari za Muziki na Mixtapes Bure Kwenye Telegram
Imekuwa ni wiki nzuri sana kwenye soko la muziki nchini Tanzania kwani wasanii tofauti tofauti wameachia ngoma kali ambazo bila shaka zimezua tabasamu kwa mashabiki. Zifuatazo ni ngoma tano mpya ambazo zimeachiwa na wasanii kutokea nchini Tanzania kwa wiki hii:
Addiction - Ibraah ft Harmonize
Baada ya kufanya vizuri na ngoma yao ya ‘One Night Stand, Ibraah na Harmonize wamerudi tena na ngoma mpya ya kuitwa ‘Addiction’. ‘Kwenye ‘Addiction’, Ibraah na Harmonize wanasifia ubora wa pombe huku wakitoa tahadhari kuhusu madhara anayoweza kupata mtu iwapo atazidisha kunywa pombe.
Safari (EP) - K2ga
Kutoka lebo ya King's Music, mwanamuziki K2ga ameachia EP yake ya kuitwa ‘Safari’ ambayo imesheheni ngoma tatu ambazo ni ‘Ni wewe’, ‘Danga’ pamoja na ‘Goma. Safari ni EP ya kwanza kutoka kwa K2ga na inategemewa kufanya vizuri sana ndani na nje ya nchi.
Baba Jeni - Maua Sama
Mdundo mkali kutoka kwa Bin Laden na Mr Simon umefanya ngoma ya ‘Baba Jeni’ kuwa bora sana. Kwenye wimbo huu, Maua Sama anatoa ya moyoni kuhusu mpenzi wake wa zamani kwa kusema kuwa hamuhitaji tena kwenye maisha yake.
Party - Nandy ft Billnass & Mr Eazi
Kwenye ngoma ya ‘Party’, Nandy anajipa kazi ya kuwapeleka watu kwenye club na sehemu za mbalimbali starehe kupitia ngoma hii. Nandy anawahasa watu kujiachia na kwenda kustarehe kwani maisha ni mafupi. Hii ni ngoma ambayo inawakutanisha kwa mara nyingine Nandy na Billnass pamoja na Mr Eazi ambaye ni msanii kutokea nchini Nigeria.
Acha Niongee - Nay Wa Mitego
Gwiji wa Hip-hop kutokea Tanzania Nay Wa Mitego amerudi tena na ngoma yake mpya ya kuitwa ‘Acha Niongee’ ambayo ndani yake ameainisha changamoto ambazo amezipitia kwenye harakati zake za muziki.
Weekly Top 10 songs
Top stories
- Playlist my upcoming song
30 March
- ITSLILREMY
30 March
- Usman Khalifa Amoto
30 March
- Ingopangani Download nyimbozi
30 March




Leave your comment